Top Songs By Bando MC
Similar Songs
Credits
PERFORMING ARTISTS
Bando MC
Performer
COMPOSITION & LYRICS
Mussa Mabumo Mussa
Songwriter
Lyrics
(Wewe) mh (wewe)
Mmh (wewe, mh-ah, wewe)
Spana, ah-mh
Shy town boy (mh)
Niko na Drama boy (mh)
(Jey Drama on the beat)
Ah, hi, hi, hi, Huddah
Uhali gani we msaliti haufai Yuda, nimeona leo nikusabahi nainai
Nilikuhongaga mpaka saa, na bado ukanipotezea muda
Ah, penzi lako kama lift ukanishushua njiani
Hukuamini kuna siku mziki utanipa ramani
Ukapata mchizi asiye na dhiki na akakuweka ndani
Hivi hukujua nyumba ya ridhiki mpangaji
Ilinitouch sana iliniumiza sana, ilinifanya nikakesha usiku na mchana
Haukuwa fungu langu kwahiyo sikuweza kung'ang'ana
Kisicho ridhiki hakiliki hata kikiungwa na nyanya
Vipi, mchizi yupo? Mbona siku hizi hampostiani tena
Makopa kopa lnstagram hamkomentiani tena
Mtaani hatuwaoni mkiongozana tena
Sitaki amini ka' na yeye tayari mmeshaachana tena
Nisingekuwa mstaamilivu
Huwenda duniani leo nisingekuwepo
Ulinipa maumivu, niliamini siwezi kupona leo wala kesho
Namshukuru Mungu, kwa kunifutia kumbukumbu zako
Maana niliishi na maumivu
Mwili ukawa kijivu, nikawa ni kichekesho
Sikulaumu wewe (wewe), sikuombei magumu wewe (wewe)
Mungu akurehemu wewe (wewe)
Unayoyafanya kwangu yasijirudie kwako, oh
Ooh, mh
Ah, usidhani nakuchukia, mi' sikuchukii (mi sikuchukii)
Hizi salamu tu nakutumia
Hata mapenzi yako mi' sikumbukii (hata mapenzi yako mi' sikumbukii)
Uliacha mbachao kwa msala upitao, kunikalia vikao haisaidii
Naskia ukinionaga kwa TV, unatamani urudi ila mimi ndo sifikirii
Ah, mshedede siku hizi na vichenchede
Mambo yako yedede, bata kila deide
Mafekeche debe daily tukiplay dede
Si ulisema sina future maisha nimeyamedede
Ah, najiona mbali, siku mziki umeshaanza kunilipa
Nashukuru Mungu bwana, kila kona nasikika
Kila dakika kote nafika
Na kwenye show siendi na dyaba, nakuwaga mapipa
Jangwani uliniacha mpenzi
Ukaenda mbali nami, ukafuata wenye maji mengi
Angani kuna nini mpenzi
Ulichagua maisha ya ndege kuruka kuspend
Utu, utu wangu niliwekeza kwako utu
Utu, utupu wako ulimuonyesha mwenye pesa
Akaenda na we, eh, we
Nisingekuwa mstaamilivu
Huwenda duniani leo nisingekuwepo
Ulinipa maumivu, niliamini siwezi kupona leo wala kesho
Namshukuru Mungu, kwa kunifutia kumbukumbu zako
Maana niliishi na maumivu
Mwili ukawa kijivu, nikawa ni kichekesho
Sikulaumu wewe (wewe), sikuombei magumu wewe (wewe)
Mungu akurehemu wewe (wewe)
Unayoyafanya kwangu yasijirudie kwako, oh
Take five now (take five now)
Lyrics powered by www.musixmatch.com