Lyrics

Yesu pendo lako ni pendo la ajabu ×3 Pendo ambalo sikupata ulimwenguni. Nilizunguka nikitafuta rafiki oh, Nikazunguka nikitafuta mpenzi Rafiki wote walikuwa ni waongo, Naye mpenzi kageuka kuwa hasidi. Waliniacha nikiwa hali mahututi, Niliodhani kuwa ni rafiki zangu, Naye mpenzi akaniharibia sifa, Yesu akaja kwa kweli kaniokoa. Yesu pendo lako ni pendo la ajabu ×3 Pendo ambalo sikupata ulimwenguni. Na kitandani nilikuwa nimelazwa, Marafiki wakanitazama kaenda, Wakasema kweli huyu hawezi pona, lakini Yesu yeye hakuniacha. Korokoroni kwa kweli mi nilipofungwa, Hakuna aliyetaka kuhusishwa nami, Hakuna ndugu aliye nitembelea, rafiki Yesu, yeye hakuniacha. Yesu pendo lako ni pendo la ajabu ×3 Pendo ambalo sikupata ulimwenguni. Na isitoshe baada ya haya yote, Kanionyesha dhambi zangu huyu mpenzi, Akaniambia nikitubu taniokoa, niweke huru kisha anipe uhai. Niliopata kwa Yesu ni ya ajabu, upendo huu sijapata bwana mwingine, Sasa natangaza wote wakafahamu, Pendo la Yesu ni pendo la ajabu.(Wanaimba) Yesu pendo lako ni pendo la ajabu ×3 Pendo ambalo sikupata ulimwenguni. Yesu pendo lako ni pendo la ajabu ×3 Pendo ambalo sikupata ulimwenguni. Yesu pendo lako ni pendo la ajabu ×3 Pendo ambalo sikupata ulimwenguni (Asante muumba) Yesu pendo lako ni pendo la ajabu ×3 Pendo ambalo sikupata ulimwenguni.
Lyrics powered by www.musixmatch.com
Get up to 2 months free of Apple Music
instagramSharePathic_arrow_out