Credits
PERFORMING ARTISTS
Remmy Ongala
Vocals
Remmy Ongala & Orchestre Super Matimila
Performer
Hasani Ayas Ayas
Guitar
Matu Dikundia Hassan
Saxophone
Lawrence Chuki Limbanga
Drums
Matimila
Percussion
Keito Kiniki
Vocals
Freddy Sengula Mwlasha
Guitar
Muhidini Kisukari Haji
Guitar
Saidi Salum Jumaine
Congas
COMPOSITION & LYRICS
Remmy Ongala
Composer
PRODUCTION & ENGINEERING
Basil Anderson
Producer
David Bottrill
Mixing Engineer
Christopher Johns
Assistant Engineer
Lyrics
Muziki asili yake wapi eeeee
Muziki ni wa nani eeeee
Muziki hakuna mwenyewe
Muziki ni mwito
Muziki ni fundisho
Muziki maombolezo kilio
Usinione nikiimba
Ukadhani ninayo furaha
Kumbe ninayo huzuni moyoni
Muziki alivyo na nguvu ulimwenguni kote
Hata makanisani wanaimba kwaya kwa kumuomba Mungu
Kumuabudu Mungu
Kwa kumsifu Mungu
Hata kukiwa sherehe za serikali,mbele ya Mwenyekiti kuhutubia
Ni Muziki unaanza kuwakusanya watu
Kumbuka Paulo na Sila waliimba gerezani Mungu amewasikia
Kumbuka Musa aliimba Muziki wa aina yake
Kuwakomboa wana wa Israeli
Waliopo utumwani katika nchi ya Misri
Kukiwa na sherehe utaimba nyimbo za furaha
Kukiwa na tabu utaimba nyimbo za masikitiko
Ukifa leo utapelekwa kaburini na nyimbo za maombolezo
Ni muziki pekee ulio na nguvu
Utawakusanya wabaya na wazuri msiku ya mwisho Mungu akitoa hukumu
Muziki sio uhuni
Kama muziki ni uhuni kwa nini unanunua kaseti
Kama muziki ni uhuni kwa nini unaomba nyimbo redioni
Kama muziki ni uhuni kwa nini kwa nini unanunua rekodi
Kama muziki ni uhuni kwa nini unacheza muziki weeee
Kama muziki ni uhuni kwa nini unafanya top ten show
Kumbuka siku ya mwisho ikifika
Kutakuwa mlio mmoja wa parapanda utawakusanya wateule wote
Walioteuliwa katika pembe nne za dunia
Siku ya mwisho Mungu akitoa hukumu,hukumu,hukumu
Hata kwa Mungu malaika wanaimba ooh
Muziki asili yake wapi eeeee
Muziki ni wa nani eeeee
Muziki hakuna mwenyewe
Muziki ni mwito
Muziki ni fundisho
Muziki maombolezo kilio
Usinione nikiimba
Ukadhani ninayo furaha
Kumbe ninayo huzuni moyoni
Muziki asili yake wapi eeeee
Muziki ni wa nani eeeee
Muziki hakuna mwenyewe
Muziki ni mwito
Muziki ni fundisho
Muziki maombolezo kilio
Usinione nikiimba
Ukadhani ninayo furaha
Kumbe ninayo huzuni moyoni
Writer(s): Remmy Ongala
Lyrics powered by www.musixmatch.com